Proverbs 28:1-6

1 aMtu mwovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayemfukuza,
bali wenye haki ni wajasiri kama simba.


2 Wakati nchi inapokuwa na uasi, inakuwa na viongozi wengi,
bali mwenye ufahamu na maarifa hudumisha utaratibu.


3 bMtu maskini amwoneaye yeye aliye maskini zaidi
ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza mazao.


4 cWale waiachao sheria huwasifu waovu,
bali wale waishikao sheria huwapinga.


5 dWatu wabaya hawaelewi haki,
bali wale wamtafutao Bwana wanaielewa kikamilifu.


6 eAfadhali maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama
kuliko tajiri ambaye njia zake ni potovu.

Copyright information for SwhKC