Proverbs 28:1-6
1 aMtu mwovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayemfukuza,bali wenye haki ni wajasiri kama simba.
2 Wakati nchi inapokuwa na uasi, inakuwa na viongozi wengi,
bali mwenye ufahamu na maarifa hudumisha utaratibu.
3 bMtu maskini amwoneaye yeye aliye maskini zaidi
ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza mazao.
4 cWale waiachao sheria huwasifu waovu,
bali wale waishikao sheria huwapinga.
5 dWatu wabaya hawaelewi haki,
bali wale wamtafutao Bwana wanaielewa kikamilifu.
6 eAfadhali maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama
kuliko tajiri ambaye njia zake ni potovu.
Copyright information for
SwhKC